Wanawake kutoka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI ) wameungana na wanawake wengine wa Mkoa wa Arusha katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Mkoa humo ambayo yanafanyika katika Viwanja vya Ngarenaro.
Wakizungumza na mwanahabari wetu, Wanawake hao wamesema wanajivunia kufanya kazi katika Taasisi ambayo ni injini ya uhifadhi kupitia tafiti za Wanyamapori ambazo hutumika kwa ustawi wa Uhifadhi na kukuza Utalii nchini.
Kauli mbiu ya siku ya wanawake mwaka huu ni
“WANAWAKE NA WASICHANA , MSINGI WA MAENDELEO JUMUISHI KUFIKIA DIRA YA 2050.”










Users Last 7 days : 658
Users This Month : 461
Total Users : 66635