
VIZIMBA VYAWANUSURU WANAWAKE NA WATOTO AMBAO WALIKUWA WAKISHAMBULIWA NA MAMBA KWA ASILIMIA 46.
Hali ya maisha ya kawaida imerejea kwa jamii ziishizo pembezoni mwa mito na maziwa baada ya Wizara ya Maliasili kupitia wataalamu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamopori Tanzania (TAWIRI) kujenga vizimba 50 katika maeneo mbalimbali nchini.
Wanawake na watoto ni wanufaika wakuu wa ujenzi huu wa vizimba, Elizabeti Majaliwa mkazi wa mguluma amesema awali waliishi kwa hofu ya kushambuliwa na mamba wakati wa kuteka maji kwa shughuli za nyumbani. Pia watoto walishambuliwa wakati wa kuogelewa ila kwa sasa wapo salama.
Mtafiti wa Mamba kutoka TAWIRI, Dkt. Iddi Lipende amesema, ujezi wa vizimba hivyo unalenga kuzuia/kupunguza athari za mamba katika jamii, hivyo kuimarisha usalama na ustawi wa jamii pamoja na kuwaifadhi mamba.
Dkt.Lipende amebainisha kwa mujibu wa utafiti wa Mwaka 2018, katika migongano kati ya binadamu na mamba Wanawake na Watoto ni waathirika wa mashambulio kwa asilimia (46-47%), wanaume huathirika kwa asilimia 11 kutokaa na shuguli za Uvuvi na asilimia 58 ya madhara ya mashambulio ya Mamba ni kifo huku wanao okolea kupata ulemavu wa kudumu.








Users Last 7 days : 610
Users This Month : 1184
Total Users : 69843