Coart_of_arm

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF NATURAL RESOURCES AND TOURISM

TANZANIA WILDLIFE RESEARCH INSTITUTE

Wildlife Research for Conservation

Category: news

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII NA KASI YA KUDHIBITI MIGONGANO BAINA YA WANYAMAPORI NA BINADAMU

Waziri wa Maliasili na utalii nchini Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kukamilisha zoezi la kuwafunga tembo viongozi wa makundi mikanda ya visukuma mawimbi (GPS COLLARS) ili kufuatilia mienendo yao na kudhibiti Migongano kati yao na binadamu.

Dkt. Kijaji amesema hayo leo 03 Machi, 2026 katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika Viwanja vya Nanenane vilivyopo Njiro jijini Arusha.

Aidha, amesema kuimarika kwa Uhifadhi wa rasilimali za wanyamapori kumechochea ukuaji wa sekta ya utalii nchini. “ idadi ya watalii imeongezeka kutoka 5,360,247 mwaka 2024 hadi watalii 5,935,561 mwaka 2025 sawa na ongezeko la asilimia 10.73” amefafanua Dkt. Kijaji

Dkt. Kijaji amesema Serikali inaendelea na mikakati ya kuhakikisha wanyamapori wanakuwa salama na watu wanakuwa salama “Wanyamapori ni rasilimali muhimu katika uchumi wa nchi ambapo kupitia utalii kumekuwa na ongezeko la fedha za kigeni kutoka Dola za Marekani Bilioni 3.9 hadi kufikia dola bilioni 4.4 sawa na ongezeko la asilimia 12.82.”

Akibainisha changamoto za sekta ya uhifadhi, amesema Kuongezeka kwa migongano baina ya binadamu na wanyamapori wakali na waharibifu kunasababisha mahusiano hasi kati ya binadamu na wanyamapori “ nielekeze kufanyika tafiti za kimkakati ili kubaini mbinu mpya za kukabiliana na changamoto hii” amehimiza Dkt.Kijaji

Aidha, amesema udhibiti wa migongano unaendelea ambapo tembo 176 viongozi wa makundi wamefungwa mikanda Ya visukuma mawimbi ili kufuatilia mienendo yao na kuthibiti uharibifu. Pia Kwa mamba na viboko tayari
vizimba 18 vimejengwa maeneo mbalimbali nchini

Read More »

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII DKT. ASHATU KIJAJI AONGOZA ZOEZI LA KUWAFUNGA TEMBO VISUKUMA MAWIMBI.

Kuelekea siku ya Wanyamapori Duniani, Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, yuko uwandani katika Pori la Akiba Mkungunero kuyafunga makindi ya Tembo Visukuma mawembi ili kufahamu muelekeo wao, kwa lengo la kuwazuia kuleta madhara kwa wananchi na mazao yao.

Zoezi hili pia ni utekelezaji wa maelekezo ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameki Nchemba ya kuwadhibiti Wanyamapori wakali na waharibifu husani Tembo.

Dkt. Kijaji ameishukuru Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan Kwa kuendelea kutoa fedha za kununua Visukuma Mawimbi, ndege nyuki pamoja na kutoa fedha Kwa Wizara na Taasisi zake ili kuendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kiuhifadhi.

Read More »